Tuesday, October 18, 2011

MURJI AMSHINDA ULEDI, MAHAKAMA YATUPILIA MBALI SHAURI LA ULEDI!

                  mbunge wa jimbo la Mtwara mjini akiteta na Mh. Nape Nauye alipotembelea Mtwara





Mahakama ya mkoa Mtwara, imetupilia mbali shauri la aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la mtwar a mjini kwa tiketi ya CUF Bw. Uledi Hassan Abdalah, la kukituhumu chama cha mapinduzi(CCM) kuwa kimechakachua kura za uchaguzi wa ubunge uliofanyika mwaka jana na kumpa ushindi mbunge wa jimbo hilo Bw. Asnen Murji.

Jaji wa mahakama hiyo mh. Selemani Saidi,  ametua uamuzi huo leo kwa madai kuwa upande wa mashtaka haukuwa na ushahidi wa kutosha hususan nyaraka.

MISS MTWARA 2011 AFARIKI DUNIA!

Mnyange aliyechukua taji la miss mtwara 2011 Rahma swai, amefariki dunia usiku wa jana kuamkia leo katika hospitali ya mkoa ligula kutokana na maradhi ya tumbo.

mrembo huyo ambae nyota ya ke ndio kwanza ilikuwa inaanza kung'aa, alifikishwa hospitalini hapo baada ya kulazwa katika zahanati ya sajora, baada ya kuona hali yake inazidi kuwa mbaya, alikimbizwa hospitali ya mkoa wa mtwara ligula ndipo ilipomfika umauti. 

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehem mahali anapostahili, jina la Bwana lihimidiwe, leo na hata milele.  Amina.