Monday, October 24, 2011

MTAZAMO WANGU JUU YA KIFO CHA GADAFI

Najua kuna baadhi ya viongozi wa dunia wanafurahia, na wale wapumbavu wa mawazo ambao wanapenda kuwa watumwa wa akili, wale wanaoshikiwa akili na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiendesha maisha yao.Lakini mimi kifo cha Gaddafi kimeniumiza na kinanitia uchungu, kwa sababu ule wakati wa kutawaliwa akili sasa ndio utashamiri.

Alikuwa kiongozi  aliyeona mbali, kitendo cha Gaddafi kutoruhusu nchi yake iingiliwe kiuchumi na super powers Nations, kiliwakera sana, ndio maana wakatafuta kila sababu ya kumtoa hata kwa mtutu ili wao wapate fursa za kuingia pale na kwa asilimia kubwa wameshafanikiwa sasa.

Sasa kaeni musikilize kama waliomuua watapelekwa ICC, na kuhusu nato je!!!??? wale mamilioni wa ndugu zetu waliowauwa wakati wanamtoa Gaddafi, watachukuliwa hatua gani na hao wanaojiita Supper Powers.

NI MTAZAMO TU JAMANI!!!!!!!!!!!!