Friday, June 22, 2012



Lady Jaydee: Ukiniona kwenye harusi usifikirie niko pale kuimba


Mwanamuziki mkongwe na mwenye mafanikio zaidi nchini Tanzania Judith Wambura aka Lady Jaydee amefunguka na kusema kile kinachomkera sana akihudhuria kwenye harusi.

Kupitia mtandao wa Twitter jana komando huyo wa muziki kama anavyojiita amesema watu humpanda kichwani pale wanapodhani popote alipo yupo kwa ajili ya kuimba tu.

“Siwaelewagi watu wanaokuona tu harusini kama mualikwa halafu wanaanza kukung'ang'aniza uimbe wakati hauko kwenye ratiba. Heshimu kazi ya mtu,” aliandika.

Aliongeza, “Halafu wanajua kushupalia hao, utasikia kidogo tu si wimbo mmoja tu, utadhani huo wimbo mtu uliurecord bure studio.”

Akon alipuuzia kumsainisha Drake kabla hajaenda YMCMB




Akon kwa hakika ana pua inayonusa vipaji, muulize tu T-Pain na Lady GagaLakini hata hivyo pamoja na kuwa hivyo kuna wakati huwa anashindwa pia kubaini madini na juzi kupitia kipindi "RapFix Live" rapper Kardinal Offishall aliweka wazi kosa alilolifanya

Nilimwambia kuhusu Drake mapema. Nilimwambia, Akon huyu dogo ni staa kwenye TV ni mkali balaa,” alisema Kardinall




Kardinal Offishall alikiona kipaji na uwezo wa Drake kabla ya YMCMB.


Kardinal, kama Drizzy, Anatokea Toronto, lakini alifanikiwa kutoka kabla ya Drake hajafahamika mwaka 2009 na mixtape yake So Far Gone
Nilikutana naye kabla hajaanza kufanya mixtape yake ya kwanza,” alisema. Kitu ambacho nakumbuka kuhusu Drake ni kama alikuwa na njaa ya kutoka kwenye uigizaji kwenda kwenye kurap



Baada ya kutoka nilienda na kumwambia Akon, “Nilikuambia”. Lakini hayo ni miongoni mwa mambo ambayo yamefanya kazi kwa Drake na YMCMB. Ana kambi nzuri

Unahisi Drake angekuwa hapo alipo kama Akon angemchukua