Monday, October 17, 2011

Diamond akabidhi msaada hospitali ya ligula mtwara

                              
MSANII anayetamba katika muziki wa kizazi kipya (Bongo Flava), Naseeb Abdul ‘Diamond’,  ametoa misaada mbalimbali yenye thamani ya sh. 3,500,000 na laki tano katika wodi ya wazazi ya  Hospitali ya Ligula Mkoa Mtwara.



Akikabidhi msaada huo, Diamond alisema  yeye kama msanii amevutiwa kutoa msaada katika wodi ya wazazi kwa kuwa watoto wanaozaliwa watakuwa mashabiki wake na watapenda kazi zake hapo baadaye.  Msaada msaada huo umefadhiliwa na Safari Radio Foundation.